Head image
Govt. Logo

Hits 26259 |  2 online

     
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Dk.Mwinyi Talib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
news phpto

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi akimuapisha Dk.Mwinyi Talib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amemuapisha Dk. Mwinyi Talib Haji kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.

Hafla hiyo ya kiapo imefanyika leo Ikulu Jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali, akiwemo Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Viongozi wa Idara Maalum za SMZ , viongozi wa serikali pamoja na wanafamilia.

Rais Dk. Mwinyi amemuapisha Mwanasheria huyo baada ya kumteua Novemba 3, mwaka huu kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu Nambari 55 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Kabla ya uteuzi huo, Dk. Haji alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Huduma za Tehama

Barua Pepe Msaada wa kisheria

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

MAHAKAMA DPP WAKFU LRC SADC IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 772, Mazizini, Zanzibar
Tel.: +255(24)2234683 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2234684 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2234689
Email: info@sheriasmz.go.tz