Head image
Govt. Logo

Hits 86458 |  3 online

     
Katibu George Kazi asema Jumuiya ya Mawakili itakayoanzishwa itakuwa ni ya kitaalaam
news phpto

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria na Ndg George Joseph Kazi amesema Jumuiya ya Mawakili itakayoanzishwa itakuwa ni ya kitalaamu itakayoendeshwa na wataalaam wenye sifa zinazohitajika kulingana na fani yao ya sheria.

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria na Ndg George Joseph Kazi amesema Jumuiya ya Mawakili itakayoanzishwa itakuwa ni ya kitalaamu itakayoendeshwa na wataalaam wenye sifa zinazohitajika kulingana na fani yao ya sheria

George Kazi ameyasema hayo alipokuwa akielezea mapendekezo juu ya umuhimu wa kuanzishwa kwa Jumuiya ya Mawakili Zanzibar kwenye semina ya uelewa kwa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ kwa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika ukumbi wa Ofisi za Serikali Gombani Chakechake Pemba

Ndugu George amesema kukosekana kwa sheria zisizo rasmi zinazosimamia kazi za Mawakili kumesababisha matatizo mengi ikiwemo kukosekana uwakilishi mzuri wenye weledi kwa wananchi wanaohitaji kusaidiwa kwenye vyombo vya sheria na ushauri wa kisheria , kukosekana kwa usimamizi mzuri wa ukusanyaji wa mapato .

Kutokana na chagamoto hizo Wizara ya Katiba na Sheria imeona ipo haja ya kuwa na Jumuiya ya Mawakili itakayoanzishwa kisheria, sheria inayokidhi haja ya matakwa ya wazanzibari kwa kuzingatia mazingira na kutatua chanagamoto zinazojitokeza katika usimamizi wa Jumuiya ya Mawakili

Huduma za Tehama

Barua Pepe Msaada wa kisheria

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

MAHAKAMA DPP WAKFU LRC SADC IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 772, Mazizini, Zanzibar
Tel.: +255(24)2234683 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2234684 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2234689
Email: info@sheriasmz.go.tz