Head image
Govt. Logo

Hits 35431 |  8 online

     
MHE WAZIRI … Tume ya kurekebisha Sheria kushirikiana na vyombo vya habari ili wananchi wapate kuifahamu.
news phpto

MHE WAZIRI … Tume ya kurekebisha Sheria kushirikiana na vyombo vya habari ili wananchi wapate kuifahamu.

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Khamis Juma Mwalim amewaomba wahariri vyombo vya habari, waandishi na watayarishaji vipindi kutumia vyema kalamu zao na kupaza sauti zao kwa kuwa mabalozi wazuri na jukwaa la kuwapasha habari wananchi, juu ya kazi zinazofanywa na Tume ya kurekebisha sheria ili jamii iweze kuifahamu na kuielewa majukumu yake

Ameyasema hayo katika semina ya kuwajengea uelewa waandishi wa habari, watayarishaji vipindi na wahariri wa vyombo mbali mbali vya habari kuhusu majukumu na kazi za Tume ya Kurekebisha sheria iliyofanyika katika ukumbi wa Bima uliopo

Mhe Khamis amesema jamii inaviamini vyombo vya habari hivyo umakini unahitajika katika kufikisha ujumbe ulio sahihi kwa vile vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kuelimisha jamii ‘nchi ni yetu sote tuwe wazalendo waandishi andikeni habari zenye uhalisia kwa kuzingatia maadili ya uandishi kwani taarifa zinazohusiana na masuala ya sheria zinahitaji umakini na uwelewa mzuri’alisisitiza

Aidha ameikumbusha Tume ya Kurekebisha sheria wajibu wa kukusanya maoni ya wananchi wakati wa kufanya mapitio ya marekebisho ya sheria mbali mbali wanazozifanyia kazi kabla ya kuwasilisha mapendekezo yake serikalini kwa kuwashirikisha na kuwashirikisha wanahabari ili Tume hio iweze kusikika na jamii kufahamu kile wanachokifanya.

Huduma za Tehama

Barua Pepe Msaada wa kisheria

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

MAHAKAMA DPP WAKFU LRC SADC IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 772, Mazizini, Zanzibar
Tel.: +255(24)2234683 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2234684 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2234689
Email: info@sheriasmz.go.tz