Hits 27164 | 2 online
Katibu KUBINGWA sheria imelazimisha tunapofanya kazi tuvitumie vyombo vya habari.
Ili Tume ya kurekebisha Sheria iweze kutambulika na kufahamika majukumu yake kwa wanachi ni lazima kuvitumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii
Katibu wa Tume ya Kurekebisha Sheria ndugu Kubingwa Mashaka Simba ameyasema hayo wakati alipokuwa akiwasilisha mada kuhusiana na chimbuko, muundo na kazi za Tume hio kwa waandishi wa habari, wahariri na watayarishaji vipindi kutoka vyombo mbalimbali vya habari.
Kubingwa amesema miongoni mwa mambo yanayozingatiwa na Tume hio ni kushajihisha majadiliano kwenye vikao vilivyoitishwa na Tume hio kwa kupitia vyombo vya habari pamoja na kuyatangaza mapitio na kupata maoni kutoka kwa jamii
Kubingwa amesema ndio Tume ya kurekebisha sheria ni Taasisi ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar iliyoanzishwa chini ya kifungu cha 3 cha sheria ya Tume ya kurekebisha Sheria namba 16/1986.